Iran yakataa pendekezo la Marekani la kusitisha mapigano

Chanzo cha picha, Reuters
Iran inasema imekataa pendekezo la Marekani la kusitisha mapigano.
Kulingana na shirika la habari la serikali la Iran IRNA, katika jibu lake la vipengele 10 Iran imekataa kusitisha mapigano na kusisitiza umuhimu wa kukomesha vita.
Inasema jibu hilo linajumuisha orodha ya madai ya Iran - "ikiwa ni pamoja na kukomesha uhasama katika eneo hilo, itifaki inayohakikisha kupita salama kupitia Mlango-Bahari wa Hormuz, pamoja na ujenzi upya na kuondolewa kwa vikwazo".
IRNA inaongeza kuwa Rais wa Marekani Donald Trump "kwa kuongeza muda wa mwisho mara kwa mara tena, amejiondoa kutoka kwa vitisho vyake vya awali."
Katika hatua nyingine Rais wa Marekani, Donald Trump, alirudia vitisho kwa Iran kwamba Marekani itaendelea kushambulia miundombinu yake ikiwa haitasalimu amri.
"Na ikiwa haitasalimu amri, haitakuwa na madaraja. Hawatakuwa na mitambo ya umeme. Hawatakuwa na chochote." Aliongeza kwamba "hataenda mbali zaidi, kwa sababu kuna mambo mengine ambayo ni mabaya zaidi kuliko hayo mawili."
"Kama ningekuwa na chaguo langu, ningependa kufanya nini? Chukua mafuta," anasema. "Kwa sababu yapo kwa ajili ya kuchukuliwa. Hakuna kitu wanachoweza kufanya kuhusu hilo. "Kwa bahati mbaya watu wa Marekani wangependa kutuona tukirudi nyumbani. Kama ingekuwa juu yangu ningechukua mafuta, ningeweka mafuta, nipate pesa nyingi na pia nitawatunza watu wa Iran."















