Habari za hivi punde, Iran ilikuwa 'karibu kumpata' mwanajeshi wa Marekani aliyepotea nchini humo – Trump

Chanzo cha picha, EPA
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba mwanajeshi aliyekuwa akitafutwa na Majeshi ya Marekani na Irani katika eneo la milimani kusini mwa Iran, nusra akamatwe na wanajeshi wa Iran.
Katika ujumbe aliouchapisha mapema leo katika ukurasa wa mtandao wa kijamii wa TRUTH SOCIAL, Rais Trump alitoa maelezo zaidi kuhusu juhudi za kumuoka mwanajeshi huyo wa pili aliyepotea Iran baada ya ndege aliyokuwa ndani aina ya F-15-E kudunguliwa siku ya Ijumaa.
“Tumemuokoa mwanajeshi huyo ambaye amejeruhiwa vibaya na aliyestahmili mazingira makali kw aujasiri. Operesheni ya kumuokoa ilitekelezwa katika eneo la ndani la milimani huko Iran. Jeshi la Iran lilikuwa linamkaribia mwanajeshi huyo na lilikuwa limetekeleza operesheni kali ya kumtafuta, kwa kutumia idadi kubwa ya wanajeshi wa ardhini na teknolojia ingawa walikuwa karibu sana kumfikia. Mwanajeshi huyo ni afisa mwenye kiwango cha Kanali anayeheshimika sana.”
'‘Aina hii ya operesheni haijawahi kutelekezwa wakati mwingine na ni nadra sana kufanyika kwa sababu ya hatari kwa binadamu na mashine ambazo hutumiwa. Operesheni ya pili, ilifanyika muda mfupi baada ya ile ya kwanza, ambapo tulimuokoa Rubani na afisa wa kwanza mchana peupe, jambo ambalo pia si la kawaida, na ilituchukuwa saa saba ndani ya himaya ya Iran.’'
“Huu ni ujasiri, na uwezo wa kutekeleza kazi ulioonyesha na wahusika wote. Nitaandaa kikao cha wanahabari kwa pamoja an Jeshi la Makerakni katika ofisi ya Rais ya Oval Jumattau saa saba mchana. Mungu aibariki Jeshi letu na Mashujaa wetu. Rais DONALD J.TRUMP”
Maelezo zaidi:









