Lamine Yamal apata jeraha
Lamine Yamal amepata majeraha wakati akipiga penalti iliyoipa Barcelona ushindi mwembamba dhidi ya Celta Viga na kuongeza kileleni mwa La Liga kwa pointi tisa.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 alifunga penalti dakika ya 40 kwenye Uwanja wa Nou Camp baada ya kuingia ndani ya eneo la hatari na kuangushwa na Yoel Lago.
Lakini mara tu baada ya kuingiza mpira wavuni kipa Lamine Yamal alikwenda chini huku ameshika paja lake la kushoto.
Alitoka uwanjani kwa msaada wa madaktari wa timu na kuelekea moja kwa moja kwenye handaki huku nafasi yake ikichukuliwa na Roony Bardghji.
Ushindi huo unawafikisha mabingwa watetezi wa La Liga, Barcelona - ambao wamebakiwa na michezo sita - kuelekea kutetea ubingwa wao.
Hansi Flick anatumai jeraha la Lamine Yamal halitamzuia kucheza mechi ya Clasico mwezi ujao dhidi ya Real Madrid iliyo katika nafasi ya pili, huku Uhispania ikiwa na wasiwasi kuhusu utimamu wa mwili wa kijana huyo kwa Kombe la Dunia mwezi Juni.
Lamine Yamal, ambaye amefunga mabao 16 na kutoa pasi 11 za mabao katika La Liga msimu huu, alitajwa kuwa Mchezaji Bora Kijana Katika Mashindano ya Euro 2024 huku Uhispania ikitwaa kombe hilo.