Moja kwa moja, Mbivu na mbichi za matukio ya Oktoba 29 kujulikana leo Tanzania

Ripoti ya Tume ya Matukio ya Oktoba 29 inachukuliwa kama nyenzo muhimu ya kuweka wazi ukweli na kutoa mwelekeo wa taifa baada ya kipindi hicho kigumu.

Moja kwa moja

Na Martha Saranga

  1. Serikali ya Zambia yachukua mwili wa rais wa zamani baada ya mvutano na familia

    cxv

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Serikali ya Zambia inasema imechukua mwili wa rais wa zamani Edgar Lungu ambaye alifariki dunia Afrika Kusini miezi 10 iliyopita, uamuzi unaoenda kinyume na matakwa ya familia yake.

    Hili ni tukio la hivi karibuni katika mvutano kuhusu nini kifanyike na mwili wa kiongozi huyo wa zamani, kufuatia mgogoro wa muda mrefu kati ya Lungu na mrithi wake, Rais Hakainde Hichilema.

    Serikali imesisitiza kuwa, kama aliyewahi kuwa mkuu wa nchi, anapaswa kupewa heshima ya kitaifa na kuzikwa pamoja na marais wengine waliomtangulia katika eneo maalum la mazishi ya marais lililopo mji mkuu, Lusaka.

    Hata hivyo, familia ya Lungu ilitaka mazishi ya faragha baada ya mazungumzo na serikali kuhusu mipango ya mazishi kuvunjika.

    Mwezi Agosti mwaka jana, mahakama ya Afrika Kusini iliamua kuwa serikali ya Zambia inaweza kuurudisha mwili huo nyumbani na kufanya mazishi ya kitaifa.

    Familia iliwasilisha rufaa kupinga uamuzi huo, lakini kuhamishwa kwa mwili huo kumefuatia “kutoweza kwao kuendelea na kesi” katika mahakama ya rufaa, kwa mujibu wa taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Zambia, Mulilo Kabesha.

    Akizungumza kwenye kituo cha habari cha YouTube nchini Zambia Jumatano jioni, msemaji wa familia ya Lungu, Makebi Zulu, alipinga madai kwamba mchakato wa rufaa ulikuwa umefikia mwisho, akisema taratibu sahihi zilifuatwa.

    Sasa mawakili wa familia wamewasilisha ombi la dharura katika mahakama kuu ya Afrika Kusini ili mwili wa rais huyo wa zamani urejeshwe katika chumba cha kuhifadhia maiti ambako ulikuwa umehifadhiwa awali.

    Soma zaidi:

  2. Ripoti ya Tume ya Matukio ya Oktoba 29 kukabidhiwa leo Tanzania

    .

    Chanzo cha picha, TUME

    Macho na masikio ya Watanzania yanaelekezwa kwenye ripoti ya Tume ya Uchunguzi inayotarajiwa kukabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan baadae hii leo.

    Hii ndiyo siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu, baada ya miezi ya maswali mazito kufuatia matukio yaliyohusiana na Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

    Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Tume, Jaji Mohamed Chande, ripoti hiyo ni matokeo ya uchunguzi wa kina uliogusa pande mbalimbali za jamii.

    Kauli za awali kutoka kwa rais zilieleza madai kuwa baadhi ya vijana waliingia mitaani kwa kushawishiwa kifedha, huku wengine wakidaiwa kufuata mkumbo bila kuelewa undani wa walichokuwa wakikifanya.

    Ripoti hii inachukuliwa kama nyenzo muhimu ya kuweka wazi ukweli na kutoa mwelekeo wa taifa baada ya kipindi hicho kigumu.

    Kwa wengi, ni fursa ya kupata majibu sahihi na kujenga imani upya kwa taasisi za nchi, huku ikibeba matumaini ya kuimarisha uwazi, haki na mshikamano wa kitaifa. Endelea kutufuatilia

    Pia unaweza kusoma:

  3. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja.