Afrika kwa picha wiki hii: Tarehe 26 Aprili- 2 May 2019

Baadhi ya picha zilizochukuliwa kutoka maeneo mbali mbali ya Afrika wiki hii:

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Ni kazi ya kujichafua katika Mji wa kati wa Mali Djenne siku ya Jumapili huku wajenzi wakisaidia kuukarabati msikiti wa kale wa Grand Mosque kwa tope

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Ijumaa usiku ilikuwa ni siku ya sherehe kwa mfanyabiashara mwanamke wa Uganda Nasasi Belinda ambaye alivalishwa taji la mwanamke mwenye umbo makubwa zaidi mjini Kampala Uganda

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mashindano yalikuwa yamepangwa kusherehekea urembo wa wanawake wa Afrika wenye maumbo makubwa ya mwili

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, nchini Libya Ijumaa, waandamanaji wanaopinga mashambulio ya wanajeshi wa kiongozi mwenye mamlaka makubwa Khalifa Haftar waliingia mitaani katika mji mkuu Tripoli...

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mpiganaji aliyekuwa akiulinda mji alichukuliwa picha na mpigapicha akicheza mchezo wa video wa vita Jumatano alipokuwa akisubiri map[ambano yanayofuata

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Katika siku hiyo hiyo , waandamanaji walikuwa mitaani katika mji mkuu wa Algerian, Algiers,kwa maandamano ya Mei mosi

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Kulikuwa na maandamano nchini Sudan pia lakini mbali na maandamano hayo katika kisiwa cha mji mkuu wa Sudan khartoum cha wiliya ya Tuti, kikundi cha wavulana kilikuwa kikifurahia mawimbi ya mto Nile.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Japo kulikuwa na joto kali kwenye jangwa hili la Morocco Jumatano wiki hii, waendesha baiskeli walishiriki katika mashindano ya milima ya baiskeli

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Jumatatu, Agiro Cavanda akiangalia uharibifu uliosababishwa na kimbunga Kenneth kweneye nyumba yao baada ya kimbunga hicho kilipiga fukwe za Msumbiji

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Tamasha la Idju Owhurie katika eneo la Warri, nchini Nigeria, liliwavutia mamia ya wanaume Jumatatu ambapo husherehekea kama wapiganaji waliokuwa wakitafuta wapenzi katika karne ya 15

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Licha ya umri wake na afya yake kutatizwa na magonjwa, Askofu Mkuu wa Afrika Kusini Desmond bado anaendelea kuonyesha tabasamu hapa ni katika tukio moja mjini Cape Town Jumamosi

Picha na : AFP, EPA na Reuters