Afrika wiki hii Kwa Picha: Aprili 27 hadi Mei 3 2018

Sehemu ya picha nzuri kote barani Afrika na waafrika kwingineko duniani wiki hii

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Siku ambayo, wasanii wa kitamaduni wakitumbuiza raia katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wanachama wa kikosi cha Ulinzi cha Sudan, wakisimama imara kumsubiri Waziri mkuu wa Ethiopia kuwasili Mjini Khartoum

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Mwanamke akitengeza nyungu ya udongo, wakati wa sherehe za ufunguzi wa siku ya utalii katika mji mkuu wa Ivory Coast, Abidjan.

Nchini Zimbabwe, kundi la mchezo wa kwata likitumbuiza raia wakati wa sherehe za kila mwaka za kimataifa za sanaa (Haifa) katika mji mkuu wa Zimbabwe, Harare

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Nchini Zimbabwe, kundi moja la mchezo wa kwata likitumbuiza raia wakati wa sherehe za kila mwaka za kimataifa za sanaa (Haifa) katika mji mkuu wa Zimbabwe, Harare.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Sherehe za kila mwaka zikionyesha kipawa maridhawa cha wanasaa wa nchi hiyo, eneo la ukanda wa Kusini mwa Bara Afrika, Uchezaji dansi, Muziki, maonyesho ya mavazi na usanii wa sanaa.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, "Mabango" kujiburudisha na kujifurahisha kwenye fremu kubwa za picha, zilizotumika kupigia picha za kibinafsi ya rununu (Selfie), wakati wa sherehe za kila mwaka za Afrikaburn, zilizofanyika eneo la Tankwa Karoo, Calvinia, Afrika Kusini.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Rais wa zamani Malawi Joyce Banda, apigwa picha katik, katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Chileka, mjini Blantyre, baada ya kurejea nyumbani kutoka uhamishoni.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Macho makavu ya askari wa Cameroon, wanapojiadaa kutoka katika doria ya usiku viungani mwa mji wa Buea, katika eneo linaloshuhudia uhasama na mizozo, Kusini Magharibi mwa nchi hiyo....

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wanajeshi wanaopambana na makundi madogo madogo ya wanaharakati wanaoshinikiza upatikanaji wa uhuru wa watu wanaozungumza lugha ya kiingereza- katika eneo moja linalopakana na Cameroon na Nigeria.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Nchini Tunisia, mwanamume mmoja anendesha baiskeli kwa madaha, akipita mchoro wa Baiskeli ukutani katika kisiwa cha Djerba...

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mbio ya baiskeli ni haraka, lakini nchini Morocco, mwendesha baiskeli amechukua muda wake kuwapungia mkono wanawake na watoto anaposhiriki mbio za kilomita 600 kama Maili (372) , katika maeneo ya milima milima ya jangwa la Titan.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mhudumu wa Hoteli akimpelekea mteja mabomba ya maji ya mchanganyiko wa (shisha), kwenye mkahawa mmoja mjini Cairo, Misri, huku mchoro mkubwa ukionekana ukutani wa nyota wa soka ya kulipwa wa timu ya kandanda ya Liverpool, raia wa Misri, Mohamed Salah.

Picha zote na AFP, Getty Images, Reuters na EPA