Kwa Picha: Watu walivyoukaribisha Mwaka Mpya wa 2018 miji mbalimbali duniani

Ulimwengu unapoendelea kusherehekea kufika kwa mwaka mpya wa 2018, sherehe za aina yake zimekuwa zikifanyika miji mbalimbali mashariki hadi magharibi.

Picha hizi ni za jinsi hali ilivyokuwa miji mbalimbali.

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images

Maelezo ya picha, Hapa ni katika ufukwe wa Nungwi visiwani Zanzibar, Tanzania. Watu hawa wanaonekana kuwa tayari sana kuukaribisha mwaka mpya wa 2018.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Yogyakarta, Indonesia, fataki zilitanda angani mshale wa saa ulipogonga saa tisa usiku

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Hapa ni katika Bandari ya Victoria nchini Hong Kong

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Jumba refu sana la Petronas Towers nalo liliangazwa kwa fataki Kuala Lumpur, Malaysia

Chanzo cha picha, Reuters / Antara

Maelezo ya picha, Tukirudi Indonesia tena, taa zenye puto ziliwashwa na kupeperushwa angani katika hekalu la Borobudur

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Na katika jumba la ghorofa la 123 la Lotte World Tower, Seoul, Korea Kusini, hali haikuwa tofauti sana

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Cairo nchini Misri, Santa Claus alipiga kengele sokoni kutangaza kufika kwa mwaka mpya

Chanzo cha picha, Reuters / Antara

Maelezo ya picha, Mjini Jakarta, eneo la katikati mwa jiji fataki zilirushwa kila pahali

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Nchini Singapore, Marina Bay ndicho kilichokuwa kitovu cha sherehe

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Marekani wakazi walikuwa miongoni mwa watu wa mwisho kuukaribisha Mwaka Mpya. Katika Times Square, New York, wawili hawa walivumilia baridi kali kuusubiri Mwaka Mpya

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Sydney Harbour, maonesho haya ya fataki maarufu sana yalikuwa miongoni mwa matukio ya kuukaribisha mwaka ambayo yalioneshwa kwenye runinga pande mbalimbali duniani

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Na mbali kidogo kusini mashariki Melbourne pia walisherehekea

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mabuddha katika hekalu la Kelaniya nchini Sri Lanka waliomba kuukaribisha Mwaka Mpya

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mjini Istanbul nchini Uturuki wakazi walijitokeza barabarani kusherehekea wakisubiri kuvuka mwaka

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Champs-Élysées mjini Paris watu walifurika kama siafu

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Jijini London saa ya Big Ben ililia mshale wake wa saa ulipogonga saa sita usiku, licha ya kwamba bado inafanyiwa ukarabati mkubwa

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Na katika ufukwe maarufu wa Copacabana, Rio de Janeiro, wengi walikusanyika kuburudika na kuukaribisha mwaka mpya kwa shangwe

.