Watu 11,000 wamekamatwa nchini Ethiopia
Chanzo cha picha, Reuters
Takriban watu 11,000 wamekamatwa kutokana na uhalifu unaohusiana na hali ya hatari iliyotangazwa nchini Ethiopia, na maandamano yenye ghasia kwa mujibu wa bodi iliyoteuliwa na serikali.
Bado haijabainika ikiwa watu hao wote bado wako kizuizizi au ikiwa baadhi yao wameachiliwa.
Mwezi Oktoba serikali ya Ethiopia ilitangaza hali ya hatari ya miezi sita kufuatia maandamano yaliyoshuhudiwa kutoka kwa makabila makubwa zaidi nchini humo.
Makabila ya Oromo na Amhara huchukua asilimia 60 ya watu wote. Wengi wao hulalamika kuwa mamlaka yamedhibitwa na kabila dogo la Tigrean.
Habari kuu
Gumzo mitandaoni
Zinazovuma zaidi
Haipatikani tena
{{rankTranslation}}