Vita vya Iran: Bei ya mafuta yatarajiwa kupanda Kenya
Wakenya wametahadharishwa kuwa bei ya mafuta huenda ikapanda, huku athari za vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati zikianza kushuhudiwa.
Bei ya bidhaa hiyo muhimu duniani imekuwa ikipanda, na serikali sasa haina budi kushughulikia hali hiyo alisema Waziri wa Fedha John Mbadi.
Kuanzia katikati ya mwezi Aprili, bei ya mafuta huenda ikakabiliwa na shinikizo kuongezaka. Hata hivyo, waziri Mbadi anasema mabilioni ya fedha zitatumika kupunguza atharu ya kupanda kwa bei ya mafuta kwa watumiaji, lakini kwa muda mfupi tu.
"Mzunguko wa sasa wa bei ya mafuta, Machi 15, 2026, hadi Aprili 14, 2026, hauwezi kuathiriwa kwa vile bidhaa husika ilitolewa kabla ya mzozo wa Mashariki ya Kati," alisema Mbadi.
Serikali, hata hivyo, inasema kuwa takriban Ksh.17 bilioni zinazoshikiliwa kwa sasa katika hazina ya uimarishaji chini ya Ushuru wa Maendeleo ya Petroli zitatumwa ili kudhibiti bei na kuwakinga watumiaji kutokana na ongezeko kubwa kwa muda wa miezi mitatu ijayo.
Serikali pia inafikiria kusitisha utozaji wa ushuru wa ziada (VAT) wa mafuta, kama hatua ya kudhibiti bei ya ya bidhaa hiyo.
Pia unaweza kusoma: