Pepsi yajiondoa kama mdhamini wa tamasha ambalo Kanye West amepangwa kuliongoza
Pepsi imetangaza kujiondoa kama mdhamini mkuu wa Tamasha la Wireless jijini London msimu huu wa joto baada ya habari kwamba Kanye West ndiye atakayeongoza tamasha hili la siku tatu.
Rapa huyo wa Marekani, ambaye sasa anajulikana kama Ye, amekosolewa sana kwa matamshi ya chuki dhidi ya Wayahudi aliyotoa katika miaka ya hivi karibuni na ambayo aliomba msamaha mnamo mwezi Januari.
Awali, Waziri Mkuu Sir Keir Starmer alisema ni jambo " la kusikitisha sana" kwamba West alikuwa amepangwa kuongoza tamasha la Wireless.
Katika maoni yaliyoripotiwa kwa mara ya kwanza na Sun on Sunday, Sir Keir alisema kwamba West alikuwa amepangiwa kuongoza tamasha hilo "licha ya matamshi yake ya awali ya chuki dhidi ya Wayahudi na kusherehekea Unazi".
"Chuki dhidi ya Wayahudi kwa namna yoyote ile ni chukizo na lazima ikabiliwe vikali popote pale inapoonekana," waziri mkuu alisema.
"Kila mtu ana jukumu la kuhakikisha Uingereza ni mahali ambapo Wayahudi wanahisi salama."
West, mwenye umri wa miaka 48, alitangazwa mapema wiki jana kuwa ndiye kiongozi wa siku zote tatu za tamasha la muziki wa ‘kufokafoka na R&B’ kaskazini mwa London litakalofanyika mnamo mwezi Julai.
Tamasha hilo linatangazwa huku Pepsi ikiwasilisha Wireless – kama mdhamini mkuu.
Pia unaweza kusoma: