Moja kwa moja, Iran yasema iko mbali na makubaliano ya amani na Marekani, huku mlango bahari wa Hormuz ukifungwa tena

Spika wa bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, anasema pande hizo mbili "hazijakaribia kufikia makubaliano ya mwisho" ya mazungumzo ya kukomesha vita na Marekani.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Lizzy Masinga

  1. Papa asema hotuba ya 'madhalimu' haikuwa ikimlenga Trump

    Papa Leo

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Papa Leo amesema hakutaka kujibizana na Donald Trump alipokosoa “madikteta” wanaotumia mabilioni ya dola kwenye vita katika hotuba aliyotoa mapema wiki hii.

    Papa huyo amesema maneno yake yaliandikwa wiki mbili kabla, “kabla kabisa ya rais kutoa maoni yoyote kunihusu.”

    Amesema haikuwa nia yake kuingia kwenye mjadala na rais huyo, jambo ambalo hapendezwi nalo.

    Donald Trump hapo awali alimshambulia Papa huyo wa kwanza kutoka Marekani, akisema ni “mbaya kwa sera za nje,” hasa baada ya Papa kukosoa operesheni ya kijeshi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

    Papa huyo, ambaye yuko kwenye ziara barani Afrika, amesema kumekuwa na “simulizi isiyo sahihi” iliyojengwa kutokana na kauli za kisiasa za Trump.

    Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance amesema anamshukuru Papa kwa ufafanuzi huo na akaongeza kuwa, ingawa mara nyingine kuna tofauti za maoni, hali halisi mara nyingi huwa ngumu zaidi kuliko inavyoonekana kwenye vyombo vya habari.

    Awali, kabla ya hotuba ya Papa kuhusu “madikteta,” Vance alikuwa ameshauri Vatican ijikite zaidi kwenye masuala ya maadili.

    Wakati wa hotuba yake nchini Cameroon siku ya Alhamisi, Papa aliwakosoa viongozi ambao "hupuuza ukweli kwamba mabilioni ya dola hutumika kwa mauaji na uharibifu, lakini rasilimali zinazohitajika kwa ajili ya uponyaji, elimu hazipatikani popote".

    "Mabwana wa vita hujifanya hawajui kwamba inachukua muda mfupi tu kuharibu, lakini mara nyingi maisha yote hayatoshi kujenga upya," alisema.

    Papa pia alilaani "mzunguko usio na mwisho wa uvunjifu wa utulivu na vifo" katika eneo "lenye damu" la Cameroon ambalo lilikuwa limekumbwa na uasi kwa karibu muongo mmoja.

    Maneno hayo yalitafsiriwa na baadhi kama marejeleo ya Trump - ambaye baadaye aliwaambia waandishi wa habari: "Papa anaweza kusema anachotaka, na mimi nataka aseme anachotaka, lakini siwezi kukubaliana naye."

    Unaweza kusoma;

  2. Marekani imesema nini kuhusu kuzuia bandari za Iran?

    Meli

    Kizuizi cha majini cha Marekani dhidi ya meli zinazoingia na kutoka bandari za Iran kimekuwa kikiendelea wikendi hii.

    Donald Trump alitangaza kizuizi hicho wiki moja iliyopita, chini ya siku moja baada ya mazungumzo marefu kati ya Marekani na Iran nchini Pakistan kushindwa kufikia makubaliano.

    Vikosi vya Marekani vilisema vitazuia au kuzirudisha meli zinazosafiri kwenda au kutoka pwani ya Iran, bila kujali utaifa.

    Marekani inatarajia kuweka shinikizo kwa Iran kwa kupunguza uwezo wake wa kufaidika na mauzo ya mafuta nje ya nchi.

    Kamanda Mkuu wa Marekani alisema wikendi hii kwamba amelazimisha meli 23 kugeuka karibu na Mlango Bahari wa Hormuz tangu kizuizi hicho kilipoanza.

    Katika chapisho la mitandao ya kijamii lililochapishwa saa moja tu iliyopita, Centcom inasema "kizuizi hicho kimesimamisha kabisa biashara ya kiuchumi inayoingia na kutoka Iran kwa njia ya bahari".

    Hata hivyo, BBC Verify ilifuatilia takribani meli nne kutoka bandari za Iran ambazo zilionekana kuvuka mstari wa kizuizi cha Marekani.

    Unaweza kusoma;

  3. Iran yasema iko mbali na makubaliano ya amani na Marekani, huku mlango bahari wa Hormuz ukifungwa tena

    Mohammad Bagher Ghalibaf

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Spika wa bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, anasema kwamba ingawa "maendeleo yamepatikana" katika mazungumzo ya kukomesha vita na Marekani, pande hizo mbili "hazijakaribia kufikia makubaliano ya mwisho".

    Ghalibaf alikuwa Pakistani wiki iliyopita kwa mazungumzo ya amani na wajumbe wa Marekani, akiwemo Makamu wa Rais JD Vance.

    Hakuna tarehe iliyowekwa kwa ajili ya duru inayofuata ya mazungumzo.

    Unaweza kusoma;

  4. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu hii leo