Milipuko katika ghala la risasi yawaua watu 13 Burundi - jeshi
Takribani watu 13 wamefariki dunia na makumi ya wengine kujeruhiwa katika misururu ya milipuko mikubwa iliyotokea katika ghala la silaha mjini Bujumbura, Burundi, jeshi linasema.
Katika taarifa yake hapo awali ili kwamba watu 57, pamoja na wanajeshi watatu, walijeruhiwa.
Nyumba na magari ya kibinafsi yaliharibiwa, huku vifaa vya kijeshi viliharibiwa katika milipuko hiyo, iliongeza.
Milipuko hiyo ilitokea Jumanne jioni katika kituo hicho, kilicho katika kitongoji cha Musaga, kufuatia hitilafu ya umeme, msemaji wa jeshi alisema hapo awali.
Vipande vya silaha vilivyolipuka vilirushwa zaidi ya kilo mita tano sawa na (maili tatu).
Hapo awali, jamaa za watu walioshuhudia tukio hilo waliiambia BBC kuwa walishuhudia vifo vinne tofauti mjini humo.
Vyanzo vya usalama vililiambia shirika la habari la AFP kwamba makumi ya watu walifariki.
Mwanamke mmoja aliiambia BBC Idhaa ya Maziwa Makuu kwamba jamaa, ambaye alikuwa amezuiliwa katika Gereza Kuu la Mpimba, alifariki baada ya bomu kupiga kituo hicho.
Wafungwa kadhaa waliokuwa katika gereza hilo lililo karibu na ghala la risasi, wameripotiwa kujeruhiwa.