Sekta ya majani chai nchini Kenya yaathirika na vita vya Iran

Chanzo cha picha, Getty Images
Usafiri wa bahari Mashariki ya Kati umeathirika kutokana na vita vinavyoendelea Iran, na hii imesababisha zaidi ya kilo millioni 8 za majani chai kusalia katika maghala ya bandari ya Mombasa nchini Kenya, kwa wiki kadhaa, na kuathiri mapato ya wakulima wanaotegemea mauzo ya chai nje ya nchi.
Mkuu wa chama cha wafanyabiashara wa majani chai Afrika Mashariki lenye kusimamia mnada wa majani chai mjini Mombasa, aliiambia shirika la habari la Reuters kuwa kuanzia tarehe 1 mwezi Machi, wamarekodi hasara ya dolla millioni 8 kila wiki.
Mkurugenzi huyo amesema hakuna majani chai yanayosafirishwa kwa sasa kuelekea Mashariki ya Kati ambayo hununua takriban 25% ya mazao ya chai ya Kenya.
Vita vinavyoendelea Iran vimeathiri usafiri wa baharini, huku meli nyingi zikisitisha usafirishaji wa bidhaa kupitia Mlango Bahari wa Hormuz na Bab el-Mandeb.
Kenya huuza zaidi ya kilo millioni 100 ya majani chai Mashariki ya Kati kila mwaka, huku sasa meli zinazopeleka chai katika taifa la Pakistan zikilazimika kutumia njia ndefu ya bahari ambayo ni ghali mno.
Vita vya Ukraine na Urusi pia viliathiri biashara ya majani chai nchini Kenya. Kabla ya vita hivyo, Urusi ilikuwa inaagiza kilo millioni 29 za majani chai kutoka Kenya, ila sasa idadi hiyo imepunguka hadi kilo millioni 5.
Pia unaweza kusoma:







