Mitumba Kenya: Kwanini nguo za mitumba zimezua mjadala Kenya?

Chanzo cha picha, Getty Images

Muda wa kusoma: Dakika 2

Mgombea urais wa Kenya Raila Odinga amepuuzilia mbali madai kwamba anataka kusambaratisha biashara ya mitumba akisema kwamba ameeleweka visivyo.

Bw. Raila alisema sekta hiyo haiwezi kufungwa kwasababu inatoa ajira kwa Wakenya wengi.

Haya yanajiri bada ya wapinzani wake kutumia kauli ya kwamba nguo za mitumba zinazovaliwa sana nchini ni za watu waliokufa.

Aliwaambia wapinzani wake wajiepushe na propaganda na kutoa wito kwa washikadau wa mitumba kuwapuuza uvumi unaoenezwa mitandaoni kuhusu kauli aliyotoa kuhusu nguo za mitimba.

Licha ya ya ufafanuzi huo kwa siku ya pili mfulululizo Wakenya wamekuwa waitumia Hashatag ya Mitumba Challenge kuelezea jinsi wamekuwa wakitegemea nguo hizo.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Huku mjadala huo ukiendela mtandaoni Raila ameahidi kuwa utawala wake utaipa nguvu sekta ya biashara ili kuhakikisha wanaoitegemea hawako nje ya biashara.

"Mitumba sio biashara ya mwisho na imetengeneza ajira kwa watu wetu wengi sana nawatetea na kuna watu

Mwanasiasa Charity ngilu ambaye pia ni Gavana wa jimbo la Kitui mashariki mwa Kenya alisema mjadala unaoendelea sasa mitandaoni kuhusu mitumba uliwahi kuangaziwa na Naibu wa Rais wa Kenya William Ruto lakini haukuangaziwa lakini Raila Odinga alipotoa kauli kuhusu nguo hizo kila mmoja anazungumzia.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Mchambuzi wa siasa za Kenya MUtahi ngunyi alisema Rwanda ilisimamisha Mitumba mwaka wa 2018. Sasa Wakenya wanaagiza mitumba kutoka Rwanda. Nguo zilizovaliwa Rwanda hadi zikachakaa. Kwa hivyo nauliza: Je, Baba alisema nini kuhusu Kicomi JEANS kutoka Kenya na mashati ya Rivatex?

Ruka X ujumbe, 3
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 3

Matamshi ya Raila kuhusu nguo za mitumba yalizua taharuki kwenye mitandao ya kijamii siku ya Jumanne.

Akizindua manifesto yake katika uwanja wa Nyayo Jumatatu usiku, kiongozi huyo wa ODM alisema kuwa nguo za mitumba zinazovaliwa na Wakenya ni za watu ambao waliokufa.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mgombea urais wa Kenya Raila Odinga

"Watu wetu wamevalia tu nguo zinazotoka nje ya nchi ambazo zilivaliwa na watu waliokufa," Raila alisema.

Raila alisema atalenga kukuza tasnia ya vitambaa nchini kwa kuwapa waagizaji mitumba kipaumbele cha kwanza katika uuzaji wa nguo zinazotengenezwa nchini.

"Mimi nasema hatumuondoi mtu nje ya biashara, tutahakikisha wanaoagiza mitumba wanapata soko la bidhaa zinazoenda kutengenezwa hapa nchini," alisema.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Rwanda ilipiga marufuku uagizwaji wa nguo za mitumba kutoka nje