Kwa picha: Wiki ya Afrika katika picha: 18-24 Machi 2022

Mkusanyiko wapicha bora za wiki kutoka Barani Afrika na maeneo mengine:

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Katika mji wa Abidjan huko Ivory Coast , mwanamke anaandaakinywaji suku ya Jumapili.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Siku moja kabla, Kundi la densi Real Boys nchi Ivory Coast, lilikuwa linafanya mazoezi mjini Abidjan.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Vigaragosi vinakaribia kuchukua nafasi kubwa katika mji mkuu wa Tunisia, Tunis, Jumanne…

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mji huo umekuwa mwenyeji wa Tamasha la Sanaa la Kimataifa la Carthage ...

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Tukio hilo limerudi baada ya kuahirishwa kwa miaka miwili kwa sababu ya janga la coronavirus.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Tamasha la jangwani limekuwa likifanyika katika mji wa kusini mwa Tunisia wa Tataouine, huku Jumatano ikishuhudia msururu wa magari ya zamani.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Siku ya Jumamosi, mpiga picha alinanasa maisha katika mitaa ya mji wa Harar wenye shughuli nyingi nchini Ethiopia…

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Hapa mtu anapumzika kando ya barabara siku hiyo hiyo.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Waendesha baiskeli wanaoshiriki katika mbio za The Cape Epic hupita kwenye mashamba ya mizabibu takriban kilomita 60 kutoka mji wa Cape Town nchini Afrika Kusini siku ya Jumatatu.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Siku ya Alhamisi, wavunaji chai wanaonekana kazini karibu na mji wa Limuru nchini Kenya.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Mtoto wa tembo akijifunika kwa udongo katika kituo cha watoto yatima cha wanyama hao karibu na mji mkuu wa Kenya, Nairobi, Jumapili.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Siku moja kabla, watu wanapigwa picha kwenye kingo za Mto Loya katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambako waasi wanapigana.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Siku ya Ijumaa, wale wanaohudhuria mkutano wa kisiasa wa kumuunga mkono rais huko Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR), wanapumzika.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Siku iliyofuata, wajenga misuli walionyesha medali zao kwenye michuano ya Ashoor Classic katika mji mkuu wa Libya, Tripoli.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Siku hiyo ya Jumamosi pia, Ebony Morrison wa Liberia alifikia alama bora ya kibinafsi katika nusu fainali ya mbio za mita 60 kuruka viunzi katika mashindano ya Ridha ya Dunia inayochezwa ndani mjini Belgrade.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Siku ya Jumatatu, mfuasi wa upinzani nchini Uganda mwenye umri wa miaka 22 anaonyesha vidole viwili alivyopoteza - anadai baada ya kuteswa na maafisa wa usalama. Shirika la Human Rights Watch lilitoa ripoti siku iliyofuata na kulaani serikali kwa kutowajibisha maafisa kwa unyanyasaji huo.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Muuzaji kando ya barabara huko Lagos akichaji simu za wateja wake siku ya Jumanne. Kupotea kwa umeme ni jambo la kawaida katika jiji hilo la Nigeria.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Siku iliyofuata, watu walionekana wakitazama tukio la moto uliozuka katika sehemu ya soko la Lagos chini ya moja ya madaraja makuu matatu ya jiji hilo...

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Ilisababisha shughuli katika Daraja la Eko kukwama huku wazima moto wakijitahidi kudhibiti moto huo.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, In Niger on the same day, a woman in the capital, Niamey, is pictured with food distributed by a Turkish group ahead of the Muslim holy month of Ramadan.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Na siku ya Jumatano pia, mpishi alipigwa picha akipika chapati katika mgahawa wake katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali.

Picha zote zina haki miliki.