Picha bora zaidi kutoka barani Afrika mwaka 2021

Mkusanyiko wa picha bora zaidi kutoka barani Afrika mwaka huu:

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Padri akiwasha uvumba katika jiji la Gondor mwezi Januari wakati wa sikukuu ya kanisa la Timek - Orthodox wa Ethiopia ambayo inaadhimisha ubatizo wa Yesu katika Mto Yordani.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Pia mwezi Januari, ibada za mwisho zilifanywa kwa rais wa zamani wa Ghana, Jerry Rawlings, ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 73 Novemba 2020 .

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Tukiwa Liberia, Mwaka Mpya huleta zawadi na tabasamu baada ya kiongozi wa jumuiya, Janet Sharty kuwagawia watoto popcorn, pipi na biskuti.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Februari ilishuhudia Mayar Sherif akiandikisha historia ya kuwa mwanamke wa kwanza wa Misri kushinda taji la Grand Slam katika mechezo wa tennis Grand Slam kutokana na utenda kazi wake mzuri katika mashindano ya Australian Open.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Flamingo waliosimama juu ya maji tulivu wanaonekana hapa kama kwenye kioo katika Ziwa Magadi, Kenya

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Figuig, mji wa uliopakwa rangi angavu katika Milima ya Atlas. Hapa ni mpaka wa Morocco na Algeria

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Na huko Uhispania, Yassine Balbzioui anapiga picha karibu na kazi yake ambayo ni sehemu ya maonyesho ya sanaa ya Morocco tangu 1950.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Ethiopian Orthodox Christians in Israel celebrate on Palm Sunday...

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wakati huo huo Francis Ngannou anarejea nyumbani Cameroon kwa kukaribishwa kishujaa, baada ya kuwa bingwa mpya wa dunia wa uzani wa juu wa karate baada ya pambano lake la UFC huko Las Vegas.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Mwezi Mei viwano vya joto vilipanda nchini Misri, watoto viungani mwa mji wa Cairo walikuwa wakituliza joto hilo kwa kupiga mbizi ndani ya Mto Nile.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wakati huohuo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo maelfu ya watu walilazimika kutoka makwao wakati Mlima Nyiragongo ulipolipuka

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Juni ilishuhudia upungufu zaidi wa nguvu za umeme nchini Afrika Kusini, Hapa Cecilia Nkosi anazungumza na mjukuu wake Smangaliso nyumbani kwao huko Soweto.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wanawake hawa wanahudhuria sherehe ya kufunguliwa tena kwa maonyesho ya mavazi mjni wakiwa wamevalia nguo za kitamaduni za Harari kutoka mashariki mwa Ethiopia,

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Na almasi hii, ilielezewa kuwa ya tatu kwa ukubwa kuwahi kupatikana nchini Botswana.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mnamo Julai waigizaji wa kike wa Chad Rihane Khalil Alio na Achouackh Abakar Souleymane - ambao wanaigiza katika Lingui, The Sacred Bonds - walipanda zulia jekundu kwenye Tamasha la Filamu la Cannes nchini Ufaransa.
Maelezo ya picha, Naledi Manyoni akimrusha binti yake, Melokuhle, kutoka kwa jengo linaloungua kufuatia ghasia kubwa kupinga kifungo cha aliyekuwa Rais Jacob Zuma nchini Afrika Kusini . Mama na binti walitoka salama.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mnamo Agosti, muogeleaji wa Misri Mohab Ishak akipiga mbizi kwenye Michezo ya Olimpiki ya Tokyo 2020 iliyocheleweshwa.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Na nchini Nigeria, Prince Tsola Emiko anatawazwa kuwa olu mpya, au mfalme, wa Warri.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Septemba inaashiria mwisho wa msimu wa mvua wa Niger na kuanza kwa tamasha la Cure Salée - ambapo Nobe Nobe,15 kutoka Ago, Djanje Haiballa,17 kutoka Fouduk na Veli Rabeo,28 pia wa Fouduk - wanapiga picha.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Wakati huo huo, nchini Misri, mavuno ya pamba yanaanza. Watoto hawa wanafurahia kucheza kwenye kwenye shamba la pamba huko Fayoum, kusini mwa Cairo, Misri

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mwimbaji wa Ufaransa na Ivory Coas Vegedream (Kulia) akitumbuiza na mmoja wa mashabiki wake kwenye jukwaa kwenye Tamasha la Muziki wa Mjini Anoumabo (Femua) mjini Abidjan

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha, Baada ya miaka 10 madarakani ikiwa ni pamoja na muhula wa tatu wenye utata, Rais wa Guinea Alpha Condé anazuiliwa na jeshi latangaza kuwa limechukuwa mamlaka - likitoa picha hii kuonyesha ni nani anayeongoza.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Mnamo Oktoba Mkenya Diana Kipyogei ashinda mbio za Boston Marathon, nchini Marekani.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Miezi hiyo pia iliadhimishwa miaka 90 ya kuzaliwa kwa Askofu Mkuu wa Afrika Kusini Desmond Tutu, wakati msanii Brian Rolfe aliporejesha picha ya kasisi huko Cape Town baada ya kuharibiwa na kashfa ya ubaguzi wa rangi. Mshindi wa Tuzo ya Nobel baadaye alikufa mnamo Desemba.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mwezi Novemba washuhudia kuendelea kwa maandamano makubwa nchini Sudan kudai utawala kamili wa kiraia kufuatia mapinduzi ya Oktoba...

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wakati uwanja mkuu wa Guinea-Bissau ndio eneo la sherehe za siku ya uhuru wa nchi hiyo.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Mwezi Disemba, mwanamume mmoja na ng'ombe wake walipanga foleni kwa ajili ya feri nchini Gambia baada ya uchaguzi wa rais ambapo Adama Barrow alishinda muhula wa pili...

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Na Wizkid na Burna Boy wanafikisha mwisho mwaka kwa onyesho la kuvutia katika O2 Arena ya London.

Images from AFP, Getty Images, Reuters and BBC