Siku ya wanawake duniani 2019: Wanawake waliyong'aa katika nyanja tofauti huulizwa maswali ya kiajabu

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, What did you say?!?

Wanariadha, madaktari wa upasuaji, wajasiriamali wa teknolojia, mawaziri, wakufunzi wa yoga na maafisa wakuu watendaji wa hadhi ya juu.

Wanawake wafuatao wameongoza katika taaluma mbali mbali.

Lakini wote wameulizwa maswali ya kushangaza kuhusiana na taalamu zao hali ambayo ingeikuwa tofauti laiti wangelikuwa wanaumu.

Wanaelezea visa vyao kupitia hashtag #IfIWasAMan:

Chanzo cha picha, Neema Kaseje

Maelezo ya picha, Neema Kaseje, Daktari wa upasuaji Kenya

Neema Kaseje

Mtaalamu wA upasuaji na muasisi wa mkurugenzi wa kundi la utafiti , mjini Kisumu, Kenya na Geneva, Switzerland

"'Tunamsubiri daktari wa upasuaji.' Nalizimika kuwafahamisha kuwa mimi daktari wa upasuaji."

Chanzo cha picha, Soledad Núñez

Maelezo ya picha, Soledad Núñez, waziri wa zamani wa makaazi nchini Paraguay

Soledad Núñez

Waziri wa zamani wa makaazi nchini Paraguay, mwanasiasa na Mhandisi

"'Wewe ni mtu mdogo sana, utafanya nini katika siasa? Utaliwa na Fisi.' Ilikua mahojiano yangu ya kwanza katika chombo cha habari baada ya kuteuliwa waziri nikiwa na miaka 31."

Chanzo cha picha, Kendal Parmar

Maelezo ya picha, Mjasiriamali wa mambo ya teknolojia Kendal Parmar

Kendal Parmar

Mwanzilishi wa kampuni ya teknolojia iliyo na makaazi yake jijini London

"'Una watoto watano na unaendesha biashara ya teknolojia. Wewe ni mkakamavu sana!' Athari ya ujumbe unaoandamana na hilo neno 'mkakamavu' ndio kitu tunastahili kukabiliana nayo?"

Chanzo cha picha, Susie Rodgers

Maelezo ya picha, Mwogeleaji Susie Rodgers

Susie Rodgers, MBE

Mwogeleaji wa olimpiki ya walemavu Uingereza

"Nakabiliwa na wakati mgumu kufanya kazi na wewe kwasababunaulizwa maswali mengi."

Chanzo cha picha, Adrian Urbano

Maelezo ya picha, Maoi Arroyo, Mwanabiashara

Maoi Arroyo

Kiongii wa FCO, Mwekezajina kufunzi wa masuala ya biashara mjini Manila, Philippines

"Hayo majikumu ni makubwa sana. Nadhani huna mpango wa kuwa na familia."

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Lisa MacCallum Mawabiashara na naibu rais wa zamani wa kampuni maarufu ya michezo, Nike

Lisa MacCallum

Mwanzilishiwa mashirika kadhaa na naibu rais wa zamani wa kampuni maarufu ya michezo, Nike na Nike exec, nchini Australia

''Je utaiwakilisha shirika katika shindano la urembo?"

Chanzo cha picha, Ayla Majid

Maelezo ya picha, Ayla Majid, Pakistani mtaalamu wa masuala ya kiuchumi

Ayla Majid

Mtaalamu wa masuala ya kiuchimi na mshauri wa kibiashara wa Pakistan

Katika mahojiano ya televisheni: "Unaweza kuendelea kufanya kazi nasi kwa muda mrefu? Biashara yetu inafanya vizuri."

Chanzo cha picha, Karen Blackett

Maelezo ya picha, Karen Blackett,mtaalamu wa mauzo na mawasiliano

Karen Blackett, OBE

Mwenyekiti wa kampuni ya MediaCom Uingereza na msimamizi wa kitaifa wa WPP Uingereza

"Kazi yako ni nzuri, lakini mafaniyo hayo ni yakibinafsi inasidia vipi kampuni...."

Chanzo cha picha, Nino Zambakhidze

Maelezo ya picha, Nino Zambakhidze ana kampuni kadhaa za usafirishaji wa bidhaa za kilimo mjini Georgia

Nino Zambakhidze

Mtaalamu wa kilimo, biashara, usafirishaji, na muanzilishi wa kanda ya biasharamjini Georgiamiongoni mwa nyingine

"Urembo wako ni silaha yako,"

Chanzo cha picha, David Hindley

Maelezo ya picha, Belinda Parmar is a tech addiction campaigner and CEO of The Empathy Business

Belinda Parmar, OBE

Mwanabiashara wa teknolojia na mkurunzi CEO shirika la biashara na sister wa Kendal

"'Belinda anajiamini sana.' Sijawahi kusikia mwanamume akizungumziwa hivyo'"

Chanzo cha picha, Richard Lawson

Maelezo ya picha, Husna LawsonMataalamu wa masuala ya mawasiliano ya kiusalama Bangladesh

Husna Lawson

Mshauri wa masuala ya usalama Bangladesh

"Unaelewa haya masuala ya uslama wa kimtandao kweli?

Chanzo cha picha, Andrea Cooper

Maelezo ya picha, Andrea Cooper mkufuzi wa yoga

Andrea Cooper

Meneja na mkufunziwa yoga nchi Uingereza

"Nashangaa sana wanaume wanapowaelezea wanawake 'nguvu ya asili''