Prince William: Azuru Tanzania ili kupiga vita ujangili

Maelezo ya picha, Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba (amevaa shati jeupe na koti jeusi )akiwa pamoja na mwanamfamle William

Mwanamfalme William wa Uingereza ameanza ziara yake ya siku tatu nchini Tanzania ikiwa sehemu ya juhudi zake katika kukabiliana na ujangili na ulanguzi wa wanyama pori.

Maelezo ya picha, Prince William yuko Tanzania kwa ajili ya kampeni dhidi ya Ujangiri

Mwanamfalme huyo ambaye yuko kwenye kampeni dhidi ya ujangili wa wanyama pori kama tembo,viboko na wanyama wengine.

Maelezo ya picha, Mwanamfalme William akiwa katika bandari ya Dar es Salaam, akifahamishwa zaidi kuhusu juhudi zinazopagwa na taifa hilo

Mwanamfalme leo ameanza ziara yake katika bandari ya Dar es salaam na ataweza kutembelea mbuga ya wanyama ya Mkomazi na atatembelea chuo cha wanyama pori kilichopo kaskazini mwa Tanzania 'College of African Wildlife Management in Kilimanjaro'.

Maelezo ya picha, Mwanamfalme atatembelea pia nchini Kenya na Namibia wiki ijayo.
Maelezo ya picha, Moja ya malengo ya ziara ya Mwanamfalme William Afrika ni kuhamasisha mkutano mkuu wa kukabiliana na ujangiri wa wanyamapori ambao utaandaliwa jijini London kati ya 11-12 Oktoba