Picha bora kutoka Afrika: 3-9 Novemba 2017

Mkusanyiko wa picha za kuvutia zaidi kutoka Afrika na kuwahusu Waafrika pande mbalimbali duniani.

Chanzo cha picha, Reuters

Jumapili, Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Welby alikuwepo katika kanisa la Kiangilikana la All Saints, Nairobi. Alikutana na Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa muungano wa upinzani wa National Super Alliance (NASA) Raila Odinga.

Chanzo cha picha, EPA

Tamasha ya kutubu na kufurahia iliadhimishwa nchini Ivory Coast siku ya Jumamosi...

Chanzo cha picha, EPA

Jamii ya N'zima wanashiriki tamasha hii iitwayo Abissa au tamasha ya kuuliza swali. Inaitwa hivi kwa sababu wao hujiuliza: Je, jamii ya N'zima inastahili kuuona mwaka mpya?...

Chanzo cha picha, EPA

Mfalme na mwanawe wanabebwa mjini Grand Bassam...

Chanzo cha picha, EPA

Wakiwa wamevalia mavazi ya waliowadhulumu mwaka uliopita, wanacheza kwa sauti za chombo cha mziki aina ya tam-tam. Punde makosa yote yamesamehewa, wanafurahia mwaka mpya.

Chanzo cha picha, AFP

Siku iyo hiyo, Lamoj ambaye ni mwanamziki wa muziki wa Afrobeat alicheza katika maonyesho ya kibiashara jijini Lagos, Nigeria.

Chanzo cha picha, AFP

Siku ya Jumapili, wakazi wa Zimbabwe wanacheza ngoma katika mkutano wa injili ulitumika kama mkutano wa siasa iliyofanyika mjini Harare...

Chanzo cha picha, AFP

Wengi wa waliohudhuria walikuwa wakristo wa tabaka mbali mbali...

Chanzo cha picha, AFP

Mrengo wa vijana wa chama tawala Zanu-PF nao walipanga mkusanyiko huu ili kuonyesha uaminifu wao kwa mke wa Rais Mugabe, Grace Mugabe...

Chanzo cha picha, AFP

Alikuwepo na mumewe mwenye miaka 93, Rais Robert Mugabe. Bi Mugabe alitoa hotuba kali huku akionekana kuendeleza juhudi za kutaka kuchukua usukani kutoka kwa mumewe.

Chanzo cha picha, EPA

Jumanne, Moustafa, 15, anabeba nyuzi katika kiwanda kilichosalia pekee katika eneo nzee la mji wa Cairo, Misri...

Salama, 76, mmiliki wa kiwanda hiki alianza kufanya kazi hii akiwa miaka 7 wakati wa utawala wa mfalme Farouk aliyesemekana kuwashika wanaume wote ambao hawakuwa wanafanya kazi.

Sasa zaidi ya miaka 70 baadaye kiwanda hiki ndicho kimesalia pekee eneo la kale la Cairo. Nyuzi hizi hutumiwa kutengeneza kamba za viatu na migodoro.

Chanzo cha picha, EPA

Salama, 76, mmiliki wa kiwanda hiki alianza kufanya kazi hii akiwa miaka 7.

Chanzo cha picha, EPA

Wavuvi nchini Libya wanatia nanga katika bandari ya Tripoli, Novemba 3, 2017.

Chanzo cha picha, Reuters

Samaki wauzwa katika soko la samaki mjini Tripoli, Libya Novemba 3, 2017

Chanzo cha picha, EPA

Picha hii ilipigwa Alhamisi, taipureta iliyo katika maonyesho yaliyofanyika katika jumba la makumbusho la polisi mjini Cape Town, Afrika Kusini.

Chanzo cha picha, EPA

Jumba hili la makumbusho pia linaonyesha mfano wa jinsi maafisa walivyokuwa karne ya 1913-1957.

Images courtesy of AFP, EPA, PA and Reuters