Muuaji wa watu 39 kwenye klabu ya Reina Istanbul akamatwa
Vyombo vya habari nchini Uturuki vimesema mshukiwa mkuu katika shambulizi la mkesha wa mwaka mpya mjini Istanbul amekamatwa.
Abdulkadir Masharipov anaaminika kufanya shambulizi hilo ambalo lilisababisha vifo vya watu 39 kwenye klabu ya usiku ya Reina.
Amekamatwa katika mtaa wa Esenyurt mjini Istanbul.
Raia wa Israel, Ufaransa, Tunisia, Lebanon, India, Ubelgiji, Jordan na Saudi Arabia walikuwa miongoni mwa waliouawa huku mamia ya watu wakijeruhiwa.
Habari kuu
Gumzo mitandaoni
Zinazovuma zaidi
Haipatikani tena
{{rankTranslation}}