Matukio yaliyovutia wengi kwa picha 2016

Chaguo letu la baadhi ya picha zilizotia fora katika kuelezea taarifa kama zilivyochukuliwa kutoka maeneo mbali mbali ya dunia katika kipindi cha mwaka 2016

Chanzo cha picha, Nacho Doce/REUTERS

Maelezo ya picha, Mwanzoni mwa mwaka dunia ilikuwa katika kipindi cha dharura cha kubaini ni vipi na kwanini kirusi cha Zika kinaweza kusababisha maafa miongoni mwa watoto wachanga wanaozaliwa Amerika kusini kwa kudumaza ukuaji wa ubongo. Brazil iliripoti visa 4,000 vya maambukizi hayo tangu Oktoba 2015 - idadi ambayo haikutarajiwa. Shirika la Afya Duniani lilitangaza hali ya dharura ya kiafya katika kushughulikia maradhi hayo.

Chanzo cha picha, Pablo Martinez Monsivais/AP

Maelezo ya picha, Rais wa Marekani Barack Obama na mkewe Michelle Obam walialikwa kujaribu kucheza densi ya taifa la Argentina , tango,katika dhifa ya kitaifa walipokuwa ziarani nchini humo mwezi Machi

Chanzo cha picha, Jonathan Bachman/REUTERS

Maelezo ya picha, Ieshia Evans, mwenye umri wa miaka 27- ambaye ni muuguzi kutoka New York, alikuwa kama kielelezo cha utetezi wa haki za maisha ya watu weusi baada ya picha yake kusambazwa .Ilichukuliwa tarehe 9 Julai alipokuwa akiandamana mjini Baton Rouge kupinga mauaji ya polisi dhidi ya watu weusi.

Chanzo cha picha, BULENT KILIC/afp

Maelezo ya picha, Wakati wa jaribio la mapinduzi lililofeli , daraja la Bosphorus mjini Istanbul lilikuwa eneo la malumbano baina ya wanajeshi wakijaribu waliofanya jaribio la mapinduzi, serikali na wafuasi wa rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan. Juhudi za kupigania eneo hilo lenye muhimu linalounganisha Ulaya na Asia zilisababisha kuibuka kwa mapigano makali baina ya pande mbili.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Njia ya vioo iliyoko inayozunguka kilima cha Tianmen mjini Hunan ilikuwa ni mojawapo ya vitu vya kushangaza vilivyowavutia watalii nchini Uchina. Njia hiyo vya vioo ilikuwa na urefu wa mita 100 . Kwa wale wasio na uoga wa kutembea kwenye njia hiyo, ni mahala pazuri pa kupata taswira nzima ya maeneo yote ya Hunan

Chanzo cha picha, Tim Ireland/AP

Maelezo ya picha, Picha ya David Bowie iliyokuwa kumbu kumbu ya mwanamuziki huyo baada ya kifo chake inatarajiwa kuorodheshwa katika samani za manispaa ili kuhakikisha inatunzwa kwa muda mrefu . Umati wa mashabiki wake walikusanyika mjini Brixton kusini mwa London, eneo alikozaliwa Bowie kusherehekea maisha na muziki wake Muimbaji huyo mwenye ushawishi alifariki kwa maradhi ya saratani tarehe 11 Januari akiwa na umri wa miaka 69.

Chanzo cha picha, Danny Moloshok/ Reuters

Maelezo ya picha, Beyonce akizindua kipindi cha tuzo la Black Entertainment Television (BET) Awards mjini Los Angeles kwa onyesho la muziki la kushtukiza la wimbo wake Freedom pamoja na Kendrick Lamar, akidensi kwenye dimbwi la maji, alishinda tuzo la video ya mwaka na la chaguo la watazamaji kwampangilio wa wimbo wake, lakini alikuwa tayari ameisha ondoka kuelekea London kwa tamasha kwa hiyo mama yake Tina Knowles alipokea tuzo kwa niaba yake.

Chanzo cha picha, Emilio Morenatti/AP

Maelezo ya picha, Takriban wahamiaji 3,800 wamefariki ama kutoweka katika bahari ya Mediterranean mwaka 2016 - mwaka mbaya wa vya wahamiaji kuwahi kushuhudiwa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi (UNHCR) limesema . Hii ilitokea licha ya kupungua kwa idadi ya wakimbizi wanaovuka bahari hiyo ikilinganishwa na 2015, ambapo vifo 3,771 viliripotiwa. Hapa wahamiaji , wengi wao kutoka Eritrea, wakiruka ndani ya maiji wakati wa operesheni ya uokozi kaskazini mwa Sabratha, Libya.

Chanzo cha picha, Ian Walton/Getty Images

Maelezo ya picha, Wakimbiaji wawili katika Olimpiki mjini Rio walisifiwa baada ya kusimama kusaidiana baada ya wanawake wote kuanguka chini wakati wa mbio za mita 5,000. kwa wanawake. Mkimbiaji wa Marekani Abbey D'Agostino akimtia moyo mkimbiaji wa d New Zealand Nikki Hamblin alipkuwa ameanguka wakati wawili hao walipogongana . Licha ya kwamba D'Agostino alionekana akichechemea ,aliweza kukimbia hatua chache baada ya kumsaidia Hamblin kuinuka kabla ya kuanguka , huku mNewsealand akirudisha shukrani kwa kumsaidia hasimu wake.

Chanzo cha picha, Cameron Spencer/Getty Images

Maelezo ya picha, Mkimbiaji maarufu wa Jamaica Usain Bolt alipata fursa ya kutabasamu mbele ya kamera huku akipata ushindi wa mbio za nusu fainali mita 100. Ni tukio lililopata umaarufu katika mitandao. Baadae alishinda finali kwa muda wa sekunde 9.81 -taji lake la tatu la mita 100 Olimpiki.

Chanzo cha picha, MAHMOUD RSLAN/afp

Maelezo ya picha, Picha ya mateso na umwagaji damu ya mtoto wa kiume wa Syria aliyeokolewa kutoka kwenye jengo lililoharibiwa mjini Aleppobaada ya mashambulio ya anga iliibua hisia kali kote duniani watu wengi wakilaani yanayoendea nchini Syria. Picha ya mvulana ambaye alitambulishwa kama Omran Daqneesh mwenye umri wa miaka mitano, aliyeketi kwenye ambilansi ilitolewa na wanaharakati na kuenezwa sana kwenye mitandao ya kijamii.

Chanzo cha picha, AMEER ALHALBI/AFP

Maelezo ya picha, Familia zilitafuta njia za kutorokea upitia majengo yaliyoporomoka kufuatia mashambulio ya anga mjini Alleppo tarehe 11 Septemba. mkataba wa usitishaji mapigano ulitarajiwa kufungua njia kwa ajili ya watoaji wa misaada ndani ya Syria, lakini Urusi iliishutumu Marekani kwa kushindwa kutimiza wajibu wakechini ya mkataba huo.

Chanzo cha picha, HEIN HTET/EPA

Maelezo ya picha, Mwezi ulikaribia dunia tukio ambalo halikuwahi kushudiwa tangu mwaka 1948. Watu mbali mbali walikusanyika katika maeneo mbali mbali ya dunia kushuhudia tukio. Mwezi huo The "supermoon" ulikuwa na mwangaza zaidi barani Asia tarehe 14 Novemba.

All photographs are copyrighted.