Trump ni 'muongo' - Iran
Shirika la habari la Fars lenye mafungamano na kikosi cha walinzi wa Mapinduzi ya Iran (IRGC) limechapisha nukuu kwenye mtandao wa Telegram kutoka kwa kamanda katika makao makuu ya kijeshi ya Iran. Nukuu inayomkosoa Rais wa Marekani, Donald Trump, kwamba amekuwa akisema uongo.
Akiandika kwa Kiajemi, Meja Jenerali Abdullahi anasema kwamba IRGC imefanikiwa kuisukuma Israel na Marekani hadi kufikia hali ya kukata tamaa na uchovu,na kuwalazimu kuomba kwa dharura kusitishwa mapigano, kwa mujibu wa Fars.
Anasema vikosi vya kijeshi visingemruhusu "rais wa Marekani muongo na mdanganyifu" "kutunga maelezo ya uongo kuhusu hali ilivyo katika uwanja wa vita haswa kuhusu Mlango Bahari wa Hormuz.
Bado haijulikani wazi ikiwa ujumbe wa Iran utaelekea Islamabad kwa duru ya pili ya mazungumzo ya amani na Marekani.
Trump hakupatanikana mara moja kuelekeza hilo, lakini mara kadhaa amekanusha kuhusu tuhuma za kudanganya, akisimamia msimamo wa Marekani kwenye mzozo huo wa Mashariki ya Kati.
BC Asia Kusini anaeleza, kuna mvutano wa kisiasa nyuma ya pazia nchini Iran, huku watu wenye msimamo mkali wakiweka shinikizo kwa wapatanishi kuchagua mzozo badala ya diplomasia.
Unaweza kusoma pia: