Matumaini ya mazungumzo ya amani Pakistan yafifia

Chanzo cha picha, Reuters
Donald Trump amejigamba kuhusu mabadiliko ya utawala huko Tehran lakini sasa anashughulika na kile anachokiita kupasuka kwa utawala.
Sasa kwa kuwa viongozi wengi wakuu wa Iran wamefariki , swali la nani anayeongoza Iran kwa sasa ni halisi zaidi, jambo linalofanya jitihada za kidiplomasia kuwa ngumu zaidi.
Huenda ni mapema kutathmini athari za hatua ya hivi karibuni ya rais, lakini dalili za awali kutoka Tehran hazionekani kuwa nzuri.
Mshauri wa spika wa bunge na pia kiongozi wa mazungumzo, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesema kuwa Trump anajaribu kuvuta muda kwa ajili ya kutekeleza shambulio jingine la kushtukiza.
Msemaji wa jeshi alirejelea onyo kwamba Iran ilikuwa tayari kushambulia ikiwa hilo litatokea.
Aidha Islamabad, mipango bado inaendelea kwa ajili ya duru nyingine ya mazungumzo, huku sehemu za jiji zikiwa bado zimefungwa. Lakini matumaini ya mkutano wiki hii yanaonekana, kwa sasa, yamefifia.





