Usitishaji mapigano Lebanon si wa uhakika kwa 100% - Israel

Chanzo cha picha, Getty Images
Balozi wa Israel katika umoja wa mataifa anasema hana uhakika kuhusu hatua ya kusogezwa mbele usitishaji mapigano kama itakomesha mzozo kati ya Israel na kundi la Hezbollah linaloungwa mkono na Iran nchini Lebanon.
"Serikali ya Lebanon haidhibiti Hezbollah," Danny Dannon anasema katika mahojiano na CNN.
"Hezbollah inatuma makombora kujaribu kuhujumu usitishaji mapigano, na Israel - tunapaswa kulipiza kisasi. Kila wakati tunapoona tishio, tunachukua hatua."
Maoni yake yanakuja baada ya mabalozi wa Israeli na Lebanon nchini Marekani kukutana katika Ikulu ya White House ambapo Trump alitangaza kuongeza wiki tatu za usitishaji mapigano baada ya siku 10 za sasa.
"Hayana uhakika wa 100%," anasema akimaanisha makubaliano mapya.
"Natumai ... kuona kwamba jeshi la Lebanon linaweza kutekeleza usitishaji huu wa mapigano."
Unaweza kusoma pia:



