Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu milioni saba wanakabiliwa na njaa Yemen
Wafanyakazi wa mashirika ya misaada waliopo nchini Yeman wamesema kuwa watu wapatao million saba wanakabiliwa na baa la njaa nchini humo.
Shirika la chakula Duniani WFP limesema kuwa asilimia 60 ya raia wa taifa hilo hawana uhakika wa kupata mlo na kushindwa kujua kuwa chakula kitatoka wapi.
Hali hii imesababishwa na mapigano ya miaka miwili kati serikali ya Yemen na waasi wa Houthi hali ilisababisha hali mbaya katika huduma za kibinadamu.
Janga hilo la njaa pia linachangiwa na kuzuka kwa ugonjwa wa kipindupindu ulioathiri mamia kwa maelfu ya raia, ikiwa ni pamoja na kusababisha vifo kwa watu 200.
Madaktari wameiambia BBC kutoka mjini Yemen kuwa taifa hilo lipo hatarini kupoteza watoto nusu million kutokana na ugonjwa wa utapia mlo.