Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Marekani na Iran zamtafuta rubani wa pili wa ndege iliyoangushwa

Wataalamu wa masuala ya kijeshi wanaeleza kuwa operesheni kama hizi ni hatari sana na zinahitaji kufanyika kwa haraka zaidi

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Martha Saranga

  1. Israel yadai kushambulia 'miundombinu muhimu' ya Tehran

    Jeshi la Israel (IDF) linasema limekamilisha "wimbi la mashambulizi dhidi ya maeneo ya miundombinu ya utawala wa kigaidi" mjini Tehran siku ya Ijumaa.

    Taarifa mpya ya jeshi inasema ilishambulia eneo la ulinzi wa anga ambapo "makombora yaliyokusudiwa kulenga ndege yalihifadhiwa" pamoja na eneo la kijeshi "linalohusika na kuhifadhi taarifa za kitafiti za utawala".

    "Mashambulizi haya yaliyokamilika ni sehemu ya awamu inayoendelea dhidi ya mifumo na misingi muhimu ya utawala wa kigaidi wa Iran," IDF inasema.

    Awali iliarifiwa kwamba jeshi la Israel linasitisha kwa muda mashambulizi yake dhidi ya kusini mwa Iran, wakati juhudi za kumtafuta mwanajeshi wa ndege ya kivita ya Marekani aliyepotea zikiendelea.

    Wakati huo huo, milipuko mikubwa imesikika mashariki mwa mji wa Tehran, kwa mujibu wa vyanzo viwili, alisema mwandishi mwandamizi wa BBC Persian.

    Zaidi ya watu watatu pia wameiambia BBC kwamba wamesikia ndege za kivita zikiruka angani.

    Vyombo vya habari vya Iran vimeripoti kuwa mifumo ya ulinzi wa anga imewashwa katika mji huo.

  2. Iran imeangusha ndege vita ya pili ya Marekani

    Iran imethibitisha kuiangusha ndege ya pili ya kivita ya Marekani katika Ghuba ya Uajemi.

    Hata hivyo, vyombo vya habari vya Marekani vinaripoti kuwa ndege ya kivita aina ya A-10 Warthog ililengwa ilipokuwa katika operesheni ya uokoaji wa ndege ya kwanza iliyokuwa imeangushwa.

    Mmoja wa wahudumu wa ndege ya kivita aina ya F-15 iliyodunguliwa ameokolewa, lakini rubani bado hajulikani alipo.

    Ikiwa rubani huyo ambaye ni mwanajeshi atakamatwa na Iran, hali hiyo itaongeza mvutano mkubwa kati ya nchi hizo mbili.

    Vita hii pia imekuwa na ukosoaji mkubwa, ndani ya Marekani na kimataifa, kwamba rais wa Marekani Donald Trump hajatoa sababu thabiti ya kuanzisha vita hiyo, wala hajafanikiwa kufikia lengo lake la kubadilisha uongozi wa Iran.

    Trump amesema kuwa tukio la ndege hiyo kuangushwa halitaathiri mazungumzo na Iran.

    Hata hivyo, hali inaweza kubadilika haraka ikiwa mwanajeshi huyo atakamatwa.

  3. Marekani yamsaka rubani wake baada ya ndege kudunguliwa, Iran yatangaza dau nono

    Ripoti zinaonyesha kuwa Marekani na Iran zinashindana kwa kasi kumtafuta rubani wa pili wa ndege ya kivita ya Marekani iliyodunguliwa katika eneo la kusini mwa Iran.

    Operesheni hiyo imekuwa ya dharura huku pande zote zikijaribu kumfikia mhudumu huyo kabla ya mwingine.

    Hapo awali, uchunguzi wa BBC Verify ulithibitisha video iliyokuwa ikisambaa mtandaoni ikionyesha kile kinachoonekana kuwa ndege ya Marekani ikifuatana na helikopta mbili, zikifanya operesheni ya utafutaji na uokoaji.

    Video hiyo ilithibitishwa kushambuliwa katika jimbo la Khuzestan, karibu na daraja juu ya mto Karun.

    Video hiyo imechunguzwa ili kuthibitisha kuwa ni ya hivi karibuni na pia kuangaliwa kama ina dalili zozote za kutengenezwa kwa teknolojia ya AI, lakini hakuna ushahidi uliopatikana unaoonyesha udanganyifu.

    Hii inaongeza uzito wa taarifa kuwa operesheni hiyo ni halisi.

    Kwa mujibu wa ripoti kutoka Marekani, zikimnukuu maafisa wasiotambulishwa majina, operesheni hiyo imefanikiwa kumwokoa mmoja wa wahudumu wa ndege hiyo, lakini juhudi bado zinaendelea kumtafuta rubani wa pili ambaye hajapatikana.

    Wataalamu wa masuala ya kijeshi wanaeleza kuwa operesheni kama hizi ni hatari sana na zinahitaji kufanyika kwa haraka zaidi.

    James Jeffrey, mwanadiplomasia wa zamani wa Marekani, amesema kuwa hii ni miongoni mwa oparesheni hatari zaidi za kijeshi, kwani hujumuisha helikopta, ndege za kuongeza mafuta angani, na ndege za kulinda eneo hilo.

    Kwa upande mwingine, mhudumu na rubani wa ndege walioanguka huwa wamefunzwa kukabiliana na hali kama hizi.

    Kipaumbele chao kikuu ni kubaki hai na kuepuka kukamatwa, ikiwa ni pamoja na kujificha na kuondoka haraka katika eneo walipoangukia.

    Aidha, hupatiwa mafunzo ya mbinu za kuishi mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kupata chakula na maji au kuhimili bila hivyo kwa muda.

    Hii huwasaidia kuongeza nafasi ya kuokolewa kabla hawajapatikana na maadui.

    Unaweza kusoma pia:

  4. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu za leo.