Walemavu nchini Kenya washerehekea siku ya Valentines

Hawa ni baadhi ya watu wanaoishi na ulemavu mmoja au mwengine nchini Kenya, lakini hilo halijakuwa kikwazo maishani mwao kwani wamejumuika pamoja kuadhimisha siku ya Valentines

Maelezo ya picha, Wanakabiliwa na ulemavu wa ngozi lakini hilo halijawanyima nafasi ya kuonesha urembo wao.
Maelezo ya picha, Tabasamu la kusema usijinyime raha kwa kuwa huna uwezo wa kutumia miguu yako.
Maelezo ya picha, Changamoto kuu inayowakabili watu wenye ulemavu ni kumpata mtu atakayewapenda jinsi walivyo.
Maelezo ya picha, Baadhi ya wageni waolikwa walijumuika na pamoja na walemavu kusherehekea siku ya valentines.
Maelezo ya picha, Kinamama walivalia mavazi ya rangi nyekundu kuashiria mapenzi.
Maelezo ya picha, Baadhi ya walemavu wanahisi kuwa watu wanawapenda kupitia kile kitu walichonacho, lakini sio mapenzi ya kutoka kwa moyo.
Maelezo ya picha, Mmoja kati ya wapenzi hawa hana ulemavu lakini wanakiri kuwa unyanyapaa kutoka kwa watu ambao wana viungo vyote bado ni changamoto kwao

Chanzo cha picha, Moses Oyugi

Maelezo ya picha, Mmjo wa wageni akifuatilia mambo katika simu yake ya mkononi.

Chanzo cha picha, Moses Oyugi

Maelezo ya picha, Kila mwaka tarehe 14 Mwezi Februari watu kote duniani wanasherehekea siku ya wapendanao. waandalizi wa hafla hii walilenga kuweka tabasabu nyusoni mwa watu wenye ulemavu msimu huu wa mahaba.

Chanzo cha picha, Moses Oyugi

Maelezo ya picha, Josephita Mukhobe, katibu katika wizara ya mipango maalum nchini Kenya, anakata keki ya kuadhimisha siku ya Valentines.
Maelezo ya picha, Antony Mureithi,46 alipatwa na ugonjwa wa kupooza akiwa na miaka miwili hali ambayo ilimkosesha uwezo wake wa kutembea.