Kwa Picha: Moto mkubwa waathiri California, Marekani

Maelfu ya watu wamelazimika kukimbilia usalama wao katika maeneo yanayokuzwa mizabibu kaskazini mwa California baada ya moto mkubwa wa nyikani kuzuka maeneo hayo.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Idara ya kuzima moto jimbo hilo imesema moto unawaka maeneo 14 tofauti katika wilaya za Napa, Sonoma na Yuba.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Baadhi ya watu walijaribu kuokoa nyumba na mali yao kwa kujaribu kuzima moto huo, ambao umeathiri eka 49,000 (hekari 20,000).

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wilaya za Napa, Sonoma na Yuba hujumuisha eneo maarufu za mizabibu California na hupatikana kaskazini mwa San Francisco.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Nyumba zaidi ya 1,500 zimeteketea, mkuu wa idara ya misitu na kinga dhidi ya moto California Kim Pimlott, amesema.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Watu zaidi ya 10 wamefariki na wengine wengine wengi kujeruhiwa.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Gavana wa California ametangaza hali ya dharura katika maeneo hayo na kusema moto huo unatishia maelfu ya nyumba.ousands of residents".

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Moto huo ni miongoni mwa visa vibaya zaidi vya moto katika jimbo hilo.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Moto huo umezidishwa kasi na upepo mkubwa pamoja na kiangazi.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Chanzo cha moto huo bado hakijabainika.