Mamlaka ya
Ulinzi wa Raia na ambulensi ya Oman inazima moto uliotokea kwenye maeneo kadhaa
ya kuhifadhia mafuta katika bandari ya Salalah, vyombo vya habari vya serikali
vinasema.
Vyombo hivyo
vilisema kwamba maeneo ya mafuta yalishambuliwa na ndege zisizo na rubani.
Operesheni
za kuzima moto ziliendelea, Shirika la Habari la Oman linaloendeshwa na
serikali liliripoti, lakini "huenda ikachukua muda" kuudhibiti moto
huo.
Mamlaka
ya Iraq yasema mtu mmoja amefariki baada ya meli za mafuta kushambulia
Milipuko imeripotiwa
kwenye meli mbili za mafuta za kigeni katika Ghuba ya Uajemi karibu na bandari
ya Basra.
Mkuu wa
Kampuni Kuu ya bandari za Iraq anasema imewaokoa wafanyakazi 38 kutoka kwenye
meli hizo, na mtu mmoja amefariki, katika maoni yaliyonukuliwa na shirika la
habari la Iraq. Shughuli za utafutaji na uokoaji zinaendelea.
Tovuti za
kufuatilia meli zinaonyesha meli mbili za mafuta zinazoshukiwa kushambuliwa
zikiwa zimezungukwa na boti za uokoaji.
Chanzo cha
usalama cha Iraqi huko Basra kiliambia CNN kwamba boti ya Iran iliyojaa
vilipuzi inadhaniwa kushambulia meli hizo mbili, hata hivyo, chanzo hicho
kiliongeza kuwa uchunguzi unaendelea.
Mamlaka ya
Iraq yasema bandari za mafuta zimesimamisha shughuli zake kufuatia shambulio
hilo.
Hapo
awali, jeshi la wanamaji la Oman liliwaokoa mabaharia 20 kutoka
kwenye meli yenye bendera ya Thailand iliyoshambuliwa katika Mlango-Bahari wa
Hormuz, yapata maili 13 za baharini (kilomita 24) kutoka pwani ya Oman,
kulingana na shirika la habari la serikali la nchi hiyo.