Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda - Tanzania waanza
Ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda - Tanzania waanza
Tanzania na Uganda zimeanza kutekeleza ujenzi wa bomba la mafuta ghafi lenye urefu wa zaidi ya kilomita 1,400 unaotarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2025. Mradi huo utagharimu zaidi ya dola za Marekani bilioni 5 na unatarajiwa kuzalisha zaidi ya mapipa bilioni moja kwa kipindi cha miaka 25 ijayo.